Jumanne, 24 Desemba 2013


MCHAWI ANASWA KATIKA MKUTANO WA UFUFUO NA UZIMA MOROGORO



Alama hizo hapo tatu ni za idadi ya watu aliofanikiwa kuwaua ambao walikua wameokoka mwanzoni na baadae wakarudi nyuma.
Ikiwa ni siku ya tatu ( jumanne) ya mkutano wa ufufuo na uzima unaoendelea katika viwanja vya vya shule ya sekondari ya morogoro mchawi mmoja aliyejulikana kwa jina la Fatuma amekamatwa katika mkutano huo akiwa yuko katika shughuli zake za kila siku za kichawi.

Dada huyo aliyekamatwa na Nguvu za Mungu alielezea akasema alikuwa na wenzake ambao walitumwa na bosi wao ambaye ni mchawi na mganga wa kienyeji maarufu kutoka mjini Bagamoyo wilaya ya pwani kuja katika mji wa Morogoro kuchukua miili ya watu waliokufa katika nyumba za kuhifadhia maiti za hospitali(mochuari) kwa ajili ya kitoweo.

Akizungumza alisema yeye na wenzake walipoteana walipofika karibu na hospitali ya rufaa ya mji wa Morogoro ambapo ni eneo la jirani na sehemu mkutano unapofanyika, alipofika maeneo hayo alisikia nguvu inamvuta kwa nguvu na kumpeleka asipotaka yeye ndipo alipojikuta ametua katika viwanja shule ya sekondari ya Morogoro ambapo ndipo mkutano unapofanyika

Dada huyo aliyeonekana kuwa na wasi wasi alisema tulikuja mimi na wenzangu kwa usafiri wa njia ya fisi lakini tulipokaribia hospitali sijui nini kimetokea na mimi nikasikia nguvu zinanivuta nikajikuta niko mahali hapa

ALIANZAJE UCHAWI

Akielezea jinsi alivyoanza uchawi alisema miaka kumi na tano iliyopita alikua anaumwa ndipo alipoamua kuondoka kwao Babati(Manyara) kwenda kutibiwa mkoani Pwani kwa mganga aliyejulikana kwa jina la Idi. Alipofika kwa mganga aliambiwa akachume pilini dawa Fulani na aitafune, alipofanya sawasawa na maelekezo ya yule mganga ndipo alipojiona anaanza kuingiwa na ukatili usiokuwa wa kawaida na akaanza kupata hamu ya kula wanadamu wenzake, kuanzia siku hiyo ndipo alipoanza kuagizwa na Idi kwa ajili ya kufanya shughuli za kichawi pamoja na wenzake.



Fatuma.

NAMNA ALIVYOKUWA AKITENDA KAZI

Yeye na wenzake walikuwa wanawashughulikia hasa watu ambao waliokoka na baada ya hapo wakarudi nyuma, akieleza jinsi walivyokua wakiifanya kazi hiyo alisema mtu yeyote aliyewahi kuokoka na baada ya hapo kumuacha Yesu anakuwa na majini mawili wanaotumwa kukaa ndani yake, na wachawi hawa wanapomfuata mtu huyo wanaongea nayale mapepo na wanayaagiza yamnyonge mtu huyo na mtu huyo anakufa mara moja

Katika utendaji kazi wake yeye ndiye aliyekuwa kiongozi wa kikundi chake hicho walichokuwa wanatenda shughuli hizo za kichawi.Alisema mimi niliwekwa kuwa kiongozi wa wenzangu kwasababu mimi nilikua nimefanikiwa kuwaua watu watatu waliokua wameokoka na kurudi nyuma. Kule kwenye uchawi mtu aliyefanikiwa kuwaua watu waliorudi nyuma ndie anakua na cheo kuliko wengine, mimi niliua watu ambao walikua hawajawahi kuokoka zaidi ya thelathini na waliokua wameokoka na kurudi nyuma watatu alisema dada huyo.

Akielezea alisema sisi tulikuwa na uwezo wa kuwaua watu kwa matukio tuliyokua tunayatengeneza, unaweza ukakuta mtu anatembea njiani alafu akawa kama ameumwa na nyoka lakini nyoka mwenyewe hamuoni, mtu huyo baada ya masaa machache atakufa na sababu itakuwa kwamba aliumwa na nyoka lakini sivyo tunakuwa ni sisi tumemtengenezea kifo ili tukamle nyama.

WATU ALIOWAHI KUWAUA

Alisema anakumbuka miaka mitano iliyopita alimuua mdogo wake aaliyekuwa anajulikana kwa jina la Udiyomboli, watu watatu ambao waliwahi kuokoka na kasha kurudi nyuma pamoja na wengine Zaidi ya thelathini aliowaangamiza kwa kutumia uchawi
Baada ya hapo dada huyo akiongea kwa huzuni aliomba msaada akasema, nimechoka kufanya uchawi siyapendi maisha haya na sitaki tena kurudi kule Bagamoyo.
Dada huyo tayari ameshaachana na mambo ya uchawi na amempokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake.


Ushuhuda huu kwa mujibu wa blog ya Ufufuo na Uzima

Jumatano, 18 Desemba 2013

MAKALA; Watoto wa mitaani wanavyobakwa Sumbawanga



Baadhi ya watoto wa mitaani wakiwa wamelala nje kutokana na kukosa sehemu za kulala.Baadhi yao kwa kutaka sehemu nzuri za kulala na chakula kizuri huwa tayari kufanyiwa vitendo vibaya. Picha na Mkataba
Na Mussa Mwangoka, Mwananchi
Watoto kulawitiwa ili wapate hifadhi ya kulala au kupewa chakula kizuri ni sehemu ya maisha ya baadhi ya watoto waishio mitaani mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.
Hii ni siri kubwa ambayo imejificha miongoni mwao, ili uweze kupata siri hii inakulazimu lazima ujenge uhusiano wa karibu na wa muda mrefu na watoto hao.


Watuhumiwa wakubwa wa kuwaingilia kinyume na maumbile watoto hao ni baadhi ya walinzi wanaolinda katika maduka ya biashara na vijana waliowazidi umri; vitendo hivyo vinaonekana kushika kasi.


Uchunguzi wa kina uliofanywa na Mwandishi wa makala haya kwa miezi kadhaa, umebaini kuwa vitendo vichafu vimesababisha baadhi yao kuathirika kisaikolojia hivyo kujikuta wakiona jambo hilo ni la kawaida na hulifurahia.

Jumamosi, 26 Oktoba 2013

RAIS WA BUNGE LA USWISI AELEZEA MABILIONI, MAGAZETI DAR KUFUNGIWA



Rais wa Bunge la Uswisi, Maya Graf (wa nne kushoto) akizungumza na waandishi wa habari wa magazeti ya Mwananchi na The Citizen katika mahojiano maalumu, jijini Dar es Salaam. PICHA | EMMANUEL HERMAN

Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd kupitia magazeti yake ya Mwananchi na The Citizen, yalipata fursa pekee ya kumuhoji Rais Maya Graf, kuhusiana na masuala mbalimbali ikiwamo madhumuni ya safari yake, mabilioni hayo, uwazi wa mishahara ya viongozi wa juu serikalini na uhuru wa vyombo vya habari. Mwandishi wetu, Noor Shija alikuwa mmoja wa walioshiriki kufanya mahojiano na kiongozi huyo wa kitaifa na yafuatayo ni mahojiano hayo:

Jumamosi, 12 Oktoba 2013

WIZARA YA HABARI YAKOROGANA ,NIKUHUSU MAHABASU YA MAGAZETI.




Msomaji wa Gazeti la Mwananchi akiburudika na gazeti hilo mara baada ya kuanza shughuli za uchapaji wa gazeti, kumekuwepo na sintofahamu katika Wizara ya habari ya kutoa taarifa elekezi zinazo kinzana kuhusu kufungiwa kwa gazeti la Mwananch na Mtanzania. Picha na Fidelis Felix.

Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, jana alitoa taarifa kwa umma akieleza bayana kwamba yeye ndiye aliyeliruhusu gazeti hili kuendelea kutolewa kwa njia ya mtandao (online) na Gazeti la Rai kutolewa kila siku.


Makalla alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya Idara ya Habari-Maelezo kutoa taarifa kwamba Serikali imesikitishwa na Gazeti la Mwananchi na gazeti dada la Rai, Mtanzania kukiuka masharti ya adhabu walizopewa.


Septemba 27, mwaka huu Serikali iliyafungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90.


Wakati likianza kutumikia adhabu yake, Mwananchi ambalo tayari limemaliza kuitumikia, liliendelea kutoa taarifa kwenye tovuti yake wakati Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambayo inamiliki Mtanzania ilianza kuchapisha kila siku gazeti la Rai ambalo awali lilikuwa likichapishwa kila wiki.

Jumapili, 6 Oktoba 2013

makala :HAKUNA UGUMU WA KURUDI MISRI




Ndugu zangu,

Yanayotokea katika nchi yetu kwa sasa yanatutaka tufikiri kwa bidii. Kama nchi kuna safari tumeifunga. Na tulivyo Waafrika, tu mahodari wa kufunga safari, lakini si mahodari wa kupanga safari. Kufunga na kupanga safari ni vitu viwili tofauti.

Ndugu zangu,

Ni vigumu leo kwa Wana wa Israel kuamua kurudi tena Misri, hata kama, pamoja na chawa na kunguni walioaacha Misri, bado, kuna wanaokumbuka samaki na masufuria ya pilau waliyoayaacha Misri. Lakini, kijamii, na kwa kuingalia jamii yetu hii ilikotoka, ilipo sasa na inakoelekea, na tuone sasa, kuwa hakuna ugumu wa kurudi tena Misri. Na hapa nitazungumzia umuhimu wa sisi WaTanzania kujitambua.

Nahofia, kuwa moja ya kiini ya haya yanayotukuta sasa ni dhambi ya Ubaguzi iliyoanza kututafuna pole pole. Taratibu tunapoteza uwezo wetu wa kujitambua. Ni ukweli sasa, kuwa Watanzania hatujitambui, na kibaya zaidi, baadhi ya viongozi wetu wa kisiasa na kidini wanapoonyesha wazi wazi kuwa hawajitambui.


Maana, tumeanza sasa kuzungumza lugha za ' Wao Wakristo' na ' Sisi Waislamu'. Tunasahau, kuwa sisi ni ndugu wa damu. Kuwa SISI ni Watanzania Kwanza. Na lililo la kwanza kwetu ni ' Nchi Yetu' na maslahi yake.

Hii ni Nchi Yetu Sote. Kila Mtanzania kwa nafasi yake ana lazima ya kupigania Usalama wa Taifa letu. Usalama wa Nchi Yetu tuliyozaliwa. Hatuwezi kuilinda na kuijenga Nchi Yetu kwenye mazingira ya kubaguana. Kwenye mazingira ya kugawanyika kwa misingi ya udini, ukabila na rangi. Na hapa nitamrejea tena Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na dhana ya Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa.

Ni Mwalimu Nyerere aliyeuanzisha na kuusimamia mradi mkubwa wa Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa, hata hivyo, tunaona sasa unavyoporomoka na kuliacha taifa letu mashakani. Ndio, Mwalimu alijenga misingi imara ya Ujenzi wa Umoja Wa Kitaifa ( Nation Building).

Kuijenga jamii ya Watanzania yenye kuamini kwenye ukweli kuwa sisi sote ni ndugu. Kwamba Nchi yetu haina dini. Yenye kupiga vita ubaguzi wa aina zote, iwe wa rangi, kabila au dini. Ilimchukua Mwalimu na taifa letu miaka mingi sana kuijenga misingi hiyo iliyowawezesha pia Watanzania kuwa na mioyo ya uzalendo kwa Taifa lao.

Tunaona sasa, kazi hiyo iliyochukua miaka mingi, kutokana na ubinafsi na uroho wa madaraka ya baadhi ya wanasiasa wetu, wanapelekea kubomoka kwa misingi hiyo na kuliacha taifa letu kwenye hatari ya kuangamia.

Ndio, msingi wake ni ubaguzi wa kisiasa unaotokana na ubinafsi na tamaa ya mali kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za kufanya maamuzi makubwa kwa niaba yetu. Ni hali ya baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi kuishiwa chembe chembe za uzalendo; mapenzi kwa nchi yao.Ni watu wenye kulinda maslahi yao na ya wanaowazunguka. Wako tayari hata kutumia mbinu za Umafia kutimiza malengo yao. Kuna Watanzania wengi sasa wanaopoteza mioyo ya uzalendo kwa nchi yao.

Kuna hata wenye kufikia kutamka; 'Nchi hii ina wenyewe'. Kuna anayetamka hilo kwa lengo la kumtishia mwenzake au kulazimisha kitu fulani kifanyike. Lakini, kuna wenye kutamka hivyo kuashiria kukata tamaa. Kuwa hata wafanye nini, hakuna anayewasikiliza ama kuwajali. Hizi si dalili njema kwa taifa. Kuna wanaoiba mali ya umma mchana wa jua kali. Hakuna anayewagusa.

Ukiuliza utajibiwa; "Ah! Nchi ina wenyewe!". Kwamba kuna baadhi yetu hawajisikii kuguswa na nchi hii, hawajisikii kuwa na nguvu ya kupiga vita maovu yanayotusumbua. Baadhi yetu wameanza kupungukiwa na mapenzi na nchi yao.

Juni 16, 2004 nilipata kuandika hili kwenye gazeti la Majira; kuwa Tanzania ina vyote, kasoro Watanzania. Niliandika; kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ni nchi ya kujivunia. Kwamba Tanzania ni nchi kubwa sana kwa eneo. Ni nchi yenye rasilimali nyingi; ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, milima, mabonde, bahari na vivutio vingi vya asili.

Hata hivyo, Tanzania ni moja ya nchi masikini sana duniani. Kwa nini? Ndio, kikubwa kinachokosekana Tanzania ni Watanzania. Tanzania tunayoijenga sasa ni mkusanyiko tu wa watu wa makundi mbali mbali wenye kwenda kwa staili ya 'kila mtu na lwake'. Idadi ya Watanzania wenye uzalendo na mapenzi kwa nchi yao inazidi kupungua. Ubinafsi umekithiri, na ubinafsi mbaya zaidi ni ule wenye kufanywa na viongozi.

Ndugu zangu, Hakuna ugumu wa kurudi Misri. Tuna lazima ya kupanga safari ya kurudi tena Misri. Inawezekana.

Ni Neno la Leo.

Maggid Mjengwa,

Iringa.
0754 678 252

Slider

Sample Text

Text Widget

Jumanne, 24 Desemba 2013 0 maoni


MCHAWI ANASWA KATIKA MKUTANO WA UFUFUO NA UZIMA MOROGORO



Alama hizo hapo tatu ni za idadi ya watu aliofanikiwa kuwaua ambao walikua wameokoka mwanzoni na baadae wakarudi nyuma.
Ikiwa ni siku ya tatu ( jumanne) ya mkutano wa ufufuo na uzima unaoendelea katika viwanja vya vya shule ya sekondari ya morogoro mchawi mmoja aliyejulikana kwa jina la Fatuma amekamatwa katika mkutano huo akiwa yuko katika shughuli zake za kila siku za kichawi.

Dada huyo aliyekamatwa na Nguvu za Mungu alielezea akasema alikuwa na wenzake ambao walitumwa na bosi wao ambaye ni mchawi na mganga wa kienyeji maarufu kutoka mjini Bagamoyo wilaya ya pwani kuja katika mji wa Morogoro kuchukua miili ya watu waliokufa katika nyumba za kuhifadhia maiti za hospitali(mochuari) kwa ajili ya kitoweo.

Akizungumza alisema yeye na wenzake walipoteana walipofika karibu na hospitali ya rufaa ya mji wa Morogoro ambapo ni eneo la jirani na sehemu mkutano unapofanyika, alipofika maeneo hayo alisikia nguvu inamvuta kwa nguvu na kumpeleka asipotaka yeye ndipo alipojikuta ametua katika viwanja shule ya sekondari ya Morogoro ambapo ndipo mkutano unapofanyika

Dada huyo aliyeonekana kuwa na wasi wasi alisema tulikuja mimi na wenzangu kwa usafiri wa njia ya fisi lakini tulipokaribia hospitali sijui nini kimetokea na mimi nikasikia nguvu zinanivuta nikajikuta niko mahali hapa

ALIANZAJE UCHAWI

Akielezea jinsi alivyoanza uchawi alisema miaka kumi na tano iliyopita alikua anaumwa ndipo alipoamua kuondoka kwao Babati(Manyara) kwenda kutibiwa mkoani Pwani kwa mganga aliyejulikana kwa jina la Idi. Alipofika kwa mganga aliambiwa akachume pilini dawa Fulani na aitafune, alipofanya sawasawa na maelekezo ya yule mganga ndipo alipojiona anaanza kuingiwa na ukatili usiokuwa wa kawaida na akaanza kupata hamu ya kula wanadamu wenzake, kuanzia siku hiyo ndipo alipoanza kuagizwa na Idi kwa ajili ya kufanya shughuli za kichawi pamoja na wenzake.



Fatuma.

NAMNA ALIVYOKUWA AKITENDA KAZI

Yeye na wenzake walikuwa wanawashughulikia hasa watu ambao waliokoka na baada ya hapo wakarudi nyuma, akieleza jinsi walivyokua wakiifanya kazi hiyo alisema mtu yeyote aliyewahi kuokoka na baada ya hapo kumuacha Yesu anakuwa na majini mawili wanaotumwa kukaa ndani yake, na wachawi hawa wanapomfuata mtu huyo wanaongea nayale mapepo na wanayaagiza yamnyonge mtu huyo na mtu huyo anakufa mara moja

Katika utendaji kazi wake yeye ndiye aliyekuwa kiongozi wa kikundi chake hicho walichokuwa wanatenda shughuli hizo za kichawi.Alisema mimi niliwekwa kuwa kiongozi wa wenzangu kwasababu mimi nilikua nimefanikiwa kuwaua watu watatu waliokua wameokoka na kurudi nyuma. Kule kwenye uchawi mtu aliyefanikiwa kuwaua watu waliorudi nyuma ndie anakua na cheo kuliko wengine, mimi niliua watu ambao walikua hawajawahi kuokoka zaidi ya thelathini na waliokua wameokoka na kurudi nyuma watatu alisema dada huyo.

Akielezea alisema sisi tulikuwa na uwezo wa kuwaua watu kwa matukio tuliyokua tunayatengeneza, unaweza ukakuta mtu anatembea njiani alafu akawa kama ameumwa na nyoka lakini nyoka mwenyewe hamuoni, mtu huyo baada ya masaa machache atakufa na sababu itakuwa kwamba aliumwa na nyoka lakini sivyo tunakuwa ni sisi tumemtengenezea kifo ili tukamle nyama.

WATU ALIOWAHI KUWAUA

Alisema anakumbuka miaka mitano iliyopita alimuua mdogo wake aaliyekuwa anajulikana kwa jina la Udiyomboli, watu watatu ambao waliwahi kuokoka na kasha kurudi nyuma pamoja na wengine Zaidi ya thelathini aliowaangamiza kwa kutumia uchawi
Baada ya hapo dada huyo akiongea kwa huzuni aliomba msaada akasema, nimechoka kufanya uchawi siyapendi maisha haya na sitaki tena kurudi kule Bagamoyo.
Dada huyo tayari ameshaachana na mambo ya uchawi na amempokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake.


Ushuhuda huu kwa mujibu wa blog ya Ufufuo na Uzima Read the full story

MKURUGENZI WA KAMPUNI YA HAKI-LEO OSCAR SAMBA NA SAFU YOTE YA WAFANYAKAZI NA WANAHISA WA KAMPUNI HII WANAWATAKIA SIKUKUU NJEMA YA CHRI-MASS NA MWAKA MPYA.

Read the full story

MAKALA; Watoto wa mitaani wanavyobakwa Sumbawanga

Jumatano, 18 Desemba 2013 0 maoni



Baadhi ya watoto wa mitaani wakiwa wamelala nje kutokana na kukosa sehemu za kulala.Baadhi yao kwa kutaka sehemu nzuri za kulala na chakula kizuri huwa tayari kufanyiwa vitendo vibaya. Picha na Mkataba
Na Mussa Mwangoka, Mwananchi
Watoto kulawitiwa ili wapate hifadhi ya kulala au kupewa chakula kizuri ni sehemu ya maisha ya baadhi ya watoto waishio mitaani mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.
Hii ni siri kubwa ambayo imejificha miongoni mwao, ili uweze kupata siri hii inakulazimu lazima ujenge uhusiano wa karibu na wa muda mrefu na watoto hao.


Watuhumiwa wakubwa wa kuwaingilia kinyume na maumbile watoto hao ni baadhi ya walinzi wanaolinda katika maduka ya biashara na vijana waliowazidi umri; vitendo hivyo vinaonekana kushika kasi.


Uchunguzi wa kina uliofanywa na Mwandishi wa makala haya kwa miezi kadhaa, umebaini kuwa vitendo vichafu vimesababisha baadhi yao kuathirika kisaikolojia hivyo kujikuta wakiona jambo hilo ni la kawaida na hulifurahia.
Read the full story

RAIS WA BUNGE LA USWISI AELEZEA MABILIONI, MAGAZETI DAR KUFUNGIWA

Jumamosi, 26 Oktoba 2013 0 maoni



Rais wa Bunge la Uswisi, Maya Graf (wa nne kushoto) akizungumza na waandishi wa habari wa magazeti ya Mwananchi na The Citizen katika mahojiano maalumu, jijini Dar es Salaam. PICHA | EMMANUEL HERMAN

Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd kupitia magazeti yake ya Mwananchi na The Citizen, yalipata fursa pekee ya kumuhoji Rais Maya Graf, kuhusiana na masuala mbalimbali ikiwamo madhumuni ya safari yake, mabilioni hayo, uwazi wa mishahara ya viongozi wa juu serikalini na uhuru wa vyombo vya habari. Mwandishi wetu, Noor Shija alikuwa mmoja wa walioshiriki kufanya mahojiano na kiongozi huyo wa kitaifa na yafuatayo ni mahojiano hayo: Read the full story

WIZARA YA HABARI YAKOROGANA ,NIKUHUSU MAHABASU YA MAGAZETI.

Jumamosi, 12 Oktoba 2013 0 maoni




Msomaji wa Gazeti la Mwananchi akiburudika na gazeti hilo mara baada ya kuanza shughuli za uchapaji wa gazeti, kumekuwepo na sintofahamu katika Wizara ya habari ya kutoa taarifa elekezi zinazo kinzana kuhusu kufungiwa kwa gazeti la Mwananch na Mtanzania. Picha na Fidelis Felix.

Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, jana alitoa taarifa kwa umma akieleza bayana kwamba yeye ndiye aliyeliruhusu gazeti hili kuendelea kutolewa kwa njia ya mtandao (online) na Gazeti la Rai kutolewa kila siku.


Makalla alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya Idara ya Habari-Maelezo kutoa taarifa kwamba Serikali imesikitishwa na Gazeti la Mwananchi na gazeti dada la Rai, Mtanzania kukiuka masharti ya adhabu walizopewa.


Septemba 27, mwaka huu Serikali iliyafungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90.


Wakati likianza kutumikia adhabu yake, Mwananchi ambalo tayari limemaliza kuitumikia, liliendelea kutoa taarifa kwenye tovuti yake wakati Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambayo inamiliki Mtanzania ilianza kuchapisha kila siku gazeti la Rai ambalo awali lilikuwa likichapishwa kila wiki. Read the full story

NI WAKATI WA UKOMBOZI KWA BARA LA AFIKA,HOTU HIYO KUTOLEWA NA MWANAHARAKATI OSCAR SAMBA.

Read the full story

makala :HAKUNA UGUMU WA KURUDI MISRI

Jumapili, 6 Oktoba 2013 0 maoni




Ndugu zangu,

Yanayotokea katika nchi yetu kwa sasa yanatutaka tufikiri kwa bidii. Kama nchi kuna safari tumeifunga. Na tulivyo Waafrika, tu mahodari wa kufunga safari, lakini si mahodari wa kupanga safari. Kufunga na kupanga safari ni vitu viwili tofauti.

Ndugu zangu,

Ni vigumu leo kwa Wana wa Israel kuamua kurudi tena Misri, hata kama, pamoja na chawa na kunguni walioaacha Misri, bado, kuna wanaokumbuka samaki na masufuria ya pilau waliyoayaacha Misri. Lakini, kijamii, na kwa kuingalia jamii yetu hii ilikotoka, ilipo sasa na inakoelekea, na tuone sasa, kuwa hakuna ugumu wa kurudi tena Misri. Na hapa nitazungumzia umuhimu wa sisi WaTanzania kujitambua.

Nahofia, kuwa moja ya kiini ya haya yanayotukuta sasa ni dhambi ya Ubaguzi iliyoanza kututafuna pole pole. Taratibu tunapoteza uwezo wetu wa kujitambua. Ni ukweli sasa, kuwa Watanzania hatujitambui, na kibaya zaidi, baadhi ya viongozi wetu wa kisiasa na kidini wanapoonyesha wazi wazi kuwa hawajitambui.


Maana, tumeanza sasa kuzungumza lugha za ' Wao Wakristo' na ' Sisi Waislamu'. Tunasahau, kuwa sisi ni ndugu wa damu. Kuwa SISI ni Watanzania Kwanza. Na lililo la kwanza kwetu ni ' Nchi Yetu' na maslahi yake.

Hii ni Nchi Yetu Sote. Kila Mtanzania kwa nafasi yake ana lazima ya kupigania Usalama wa Taifa letu. Usalama wa Nchi Yetu tuliyozaliwa. Hatuwezi kuilinda na kuijenga Nchi Yetu kwenye mazingira ya kubaguana. Kwenye mazingira ya kugawanyika kwa misingi ya udini, ukabila na rangi. Na hapa nitamrejea tena Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na dhana ya Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa.

Ni Mwalimu Nyerere aliyeuanzisha na kuusimamia mradi mkubwa wa Ujenzi wa Umoja wa Kitaifa, hata hivyo, tunaona sasa unavyoporomoka na kuliacha taifa letu mashakani. Ndio, Mwalimu alijenga misingi imara ya Ujenzi wa Umoja Wa Kitaifa ( Nation Building).

Kuijenga jamii ya Watanzania yenye kuamini kwenye ukweli kuwa sisi sote ni ndugu. Kwamba Nchi yetu haina dini. Yenye kupiga vita ubaguzi wa aina zote, iwe wa rangi, kabila au dini. Ilimchukua Mwalimu na taifa letu miaka mingi sana kuijenga misingi hiyo iliyowawezesha pia Watanzania kuwa na mioyo ya uzalendo kwa Taifa lao.

Tunaona sasa, kazi hiyo iliyochukua miaka mingi, kutokana na ubinafsi na uroho wa madaraka ya baadhi ya wanasiasa wetu, wanapelekea kubomoka kwa misingi hiyo na kuliacha taifa letu kwenye hatari ya kuangamia.

Ndio, msingi wake ni ubaguzi wa kisiasa unaotokana na ubinafsi na tamaa ya mali kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za kufanya maamuzi makubwa kwa niaba yetu. Ni hali ya baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi kuishiwa chembe chembe za uzalendo; mapenzi kwa nchi yao.Ni watu wenye kulinda maslahi yao na ya wanaowazunguka. Wako tayari hata kutumia mbinu za Umafia kutimiza malengo yao. Kuna Watanzania wengi sasa wanaopoteza mioyo ya uzalendo kwa nchi yao.

Kuna hata wenye kufikia kutamka; 'Nchi hii ina wenyewe'. Kuna anayetamka hilo kwa lengo la kumtishia mwenzake au kulazimisha kitu fulani kifanyike. Lakini, kuna wenye kutamka hivyo kuashiria kukata tamaa. Kuwa hata wafanye nini, hakuna anayewasikiliza ama kuwajali. Hizi si dalili njema kwa taifa. Kuna wanaoiba mali ya umma mchana wa jua kali. Hakuna anayewagusa.

Ukiuliza utajibiwa; "Ah! Nchi ina wenyewe!". Kwamba kuna baadhi yetu hawajisikii kuguswa na nchi hii, hawajisikii kuwa na nguvu ya kupiga vita maovu yanayotusumbua. Baadhi yetu wameanza kupungukiwa na mapenzi na nchi yao.

Juni 16, 2004 nilipata kuandika hili kwenye gazeti la Majira; kuwa Tanzania ina vyote, kasoro Watanzania. Niliandika; kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana. Ni nchi ya kujivunia. Kwamba Tanzania ni nchi kubwa sana kwa eneo. Ni nchi yenye rasilimali nyingi; ardhi yenye rutuba, mito, maziwa, milima, mabonde, bahari na vivutio vingi vya asili.

Hata hivyo, Tanzania ni moja ya nchi masikini sana duniani. Kwa nini? Ndio, kikubwa kinachokosekana Tanzania ni Watanzania. Tanzania tunayoijenga sasa ni mkusanyiko tu wa watu wa makundi mbali mbali wenye kwenda kwa staili ya 'kila mtu na lwake'. Idadi ya Watanzania wenye uzalendo na mapenzi kwa nchi yao inazidi kupungua. Ubinafsi umekithiri, na ubinafsi mbaya zaidi ni ule wenye kufanywa na viongozi.

Ndugu zangu, Hakuna ugumu wa kurudi Misri. Tuna lazima ya kupanga safari ya kurudi tena Misri. Inawezekana.

Ni Neno la Leo.

Maggid Mjengwa,

Iringa.
0754 678 252 Read the full story

Sample Text

Contact

Slider

Racing

Travel

Cute

Videos

Popular Posts

My Place

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More

 
Design by NewWpThemes | Blogger Theme by Lasantha - Premium Blogger Themes | New Blogger Themes